Habari
Rais mstaafu Jakaya Kikwete na aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowasa walivyowasili kwenye msiba wa Ruge (+ Video)
Ikiwa ni siku ya pili tangu Tanzania iondokewe na mtu muhimu sana, Viongozi mbalimbali wa Serikali wameendelea kuhudhuria nyumbani kwa wazazi wake marehemu Ruge Mutahaba ambaye amefariki dunia akiwa anapokea matibabu nchini Afrika ya Kusini.
Na leo wameweza kuhudhuria baadhi ya viongozi wastaafu wakiongozwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na mke wake lakini pia aliyekuwa Waziri mstaafu Edward Ngoyai Lowasa.
By Ally Juma.