Habari
RC afuta likizo fupi za sikukuu kwa watumishi wa umma ‘kama kuna mtu ameenda mpigie simu arudi’
Mkuu wa mkoa wa Tabora, Mhe. Agrey Mwanri amefuta likizo za kipindi kifupi cha sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa watumishi wote wa umma wa mkoa wa Tabora, kwa lengo la kuhakikisha wanatatua na kukamilisha majukumu yao na kuwahudumia wananchi wenye mahitaji mbalimbali katika kipindi hiki cha mwisho wa Mwaka.
RC Mwanri akiongea kwenye kikao na watumishi wa umma mkoani humo wiki iliyopita, amewataka watumishi wote waliokua wameandaa mabegi kuondoka wasijisumbue warudi makazini isipokuwa kwa Watumishi wa Afya, Waalimu na Sekta Nyeti.
Video by rukungitz.blogspot.com