Burudani
Rick Ross akamatwa na misokoto ya bangi
Rick Ross alikamatwa Jumatano hii baada ya polisi kudaiwa kukuta misokoto mitano ya bangi kwenye gari lake.
Rapper huyo ambaye jina lake ni William Leonard Roberts II, alipelekwa Fayette County Jail, anakoshikiliwa kwa kukiuka sharti la madirisha yenye tinted.
Baada ya kulisimamisha gari lake ndipo ofisa wa polisi aliposikia harufu ya bangi ndani ya gari lake.
Ross amewahi kukamatwa mara nyingi kwa kukutwa na bangi ikiwemo tukio la Miami, 2008, in Louisiana, 2011 na North Carolina, 2013.