Lady Jay Dee
Safari ya Lady Jaydee kupanda Mlima Kilimanjaro yaanza leo
Muimbaji mkongwe nchini Tanzania, Judith Mbibo aka Lady Jaydee leo anaanza rasmi safari yake ya kupanda Mlima Kilimanjaro.Akitoa ratiba yake ya leo kupitia website yake, Jide amesema:
Tunaondokea Marangu Gate saa 3:00 asubuhi.Jumatatu ya tar 7 January 2013.
Mtiririko wa picha zaidi utakuwa unakujia kadri safari itakavyokuwa.Kama kutakuwa na network juu ya mlima. Nita post
Nifuate twitter kwa matukio live, hatua kwa hatua.Twitter.com/jidejaydee ndio anuani yangu.
Tunamtakia Jide safari njema ya kuupanda Mlima Kilimanjaro.