Technology
Samsung Galaxy S5 inaweza kuzinduliwa February 23
Wale wanaoisubiria kwa hamu simu mpya ya Samsung wanaweza wasingoje kwa muda mrefu tena. Kuna tetesi kuwa kampuni hiyo inaweza kuitambulisja Galaxy S5, Feb. 23 kabla ya Mobile World Congress, ingawa simu hiyo itaingia sokoni April.
Kwa mujibu wa Eldar Murtazin, mhariri wa mtandao wa Mobile-Review.com , simu hiyo itatangazwa mjini Barcelona Feb. 23. Hakuna taarifa za kuaminika za namna simu hiyo itakavyokuwa lakini itapewa teknolojia ya mawasiliano kati yake na macho ya mtumiaji.