Burudani

Serikali kuanzisha ‘Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa’

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iko katika mchakato wa kuanzisha ‘Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa’ ambao una dhima kubwa ya kusaidia kuinua kipato.

Naibu Waziri wa Wizara Utamaduni, Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura

Aidha mfuko huo utaongeza tija na weledi kupitia utaratibu wa upatikanaji fedha utakaowekwa ili kuwawezesha wasanii kuzalisha kazi bora za sanaa zenye kukidhi viwango vya masoko ndani na nje ya nchi.

Akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Maulid Said Mtulia aliyeuliza juu ya mpango wa serikali kuwaongezea vifaa, mitaji na menejimenti vijana walioamua kujiajiri katika sanaa mbalimbali kama vile maigizo, maonesho ya mitindo na michezo mbalimbali, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Annastazia Wambura alisema serikali yake ipo katika harakati za kuwajengea vijana mazingira mazuri ya kufanya shughuli za sanaa.

Vilevile Naibu Waziri Wambura, ameeleza kuwa katika kipindi ambacho mfuko wa maendeleo ya sanaa unaandaliwa, Serikali inashauri Halmashauri zote ziwasaidie vijana wanaojishughulisha na sanaa kwa kuwapa mikopo yenye masharti na riba nafuu kwa ajili ya mitaji kutoka kwenye asilimia 10 ya mapato ya kila Halmashauri kwa kuwa sanaa ni chanzo kikubwa cha ajira kwa vijana kwa sasa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents