Habari

Serikali yatoa neno kuhusu Bombardier na Meli ya Tanzania iliyokamatwa na dawa za kulevya

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa neno kwa mara ya kwanza kwa mwaka 2018 kuhusu ndege ya Tanzania aina ya Bombadier Q400 iliyozuliwa nchini Canada na Meli ya iliyosajiliwa kwa namba za Tanzania iliyokamatwa huko Jamhuri ya Domica na Shehena ya dawa za kulevya.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi

Kuhusu Bombardier Serikali kupitia kwa Msemaji wake Mkuu, Dkt. Abbas Hassan amesema bado ratiba ipo vile vile kuwa ndege hiyo ya Bombardier na ile kubwa ya Dreamliner zote zitafika nchini kati ya mwezi Juni na Julai mwaka huu.

Ishu ya ndege tutaizungumza itakapofika wakati wake lakini mara ya mwisho nilisema ndege zote za serikali ambazo tumenunua ratiba yake ni kufikia mwezi Juni- Julai mwaka huu ndege zote nne ikiwemo ile ndege ya ndoto yetu ya Boeing Dreamliner zitakuwa zimefika nchini.“amesema Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari.

Soma na hii – Serikali yamjibu Lissu kuhusu ujio wa Bombardier

Kwa upande mwingine Serikali imekiri kupokea taarifa za Meli yenye usajili wa Tanzania kukamatwa kwenye visiwa vya Jamhuri ya Dominika ikiwa na shehena ya dawa za kulevya aina ya Cocaine.

Suala la meli iliyokamatwa Dominika hili nalifahamu, nimelisikia kwa hiyo wenzetu wa wizara ya mambo ya nje bado wanafuatilia kujua usahihi maanake imeripotiwa hivyo kwa hiyo wizara ya nje tumeshazungumza nao na wanalifanyia kazi kwahiyo kama kutakuwa na taarifa zitatolewa.“amesema Dkt. Hassan Abbasi.

Mnamo Desemba 31, 2017 Jeshi la Maji nchini Uholanzi liliikamata Meli yenye usajili wa Tanzania ikiwa na shehena ya dawa za kulevya aina ya Cocaine tani 1.6 ambapo Meli hiyo pamoja na wahusika waliokuwemo walishikiliwa nchini Jamhuri ya Dominika kwa uchunguzi zaidi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents