BurudaniVideos

Soma jinsi Diamond alivyotaka kugoma kushoot video ya Make Me Sing baada ya hili kutokea!

Diamond si msanii anayekubali tu kirahisi kitu ambacho anahisi kinaweza kupoteza wazo lake la awali analoamini kuwa ni muhimu kufanikisha kupata zao zuri zaidi.

Hanscana amesimulia jinsi staa huyo alivyogoma kuendelea kushoot video ya wimbo wake na AKA ‘Make Me Sing’ baada ya muongozaji kutaka kurahisisha mambo:

Kipindi inashutiwa video ya make me sing by @diamondplatnumz nilijifunza vitu vingi sana ila hiki ni kimoja wapo. Tulitembea umbali kama wa km 300 hivi kwenda ku shoot zile scene Diamond anaimba kwenye white bed afu kati kati ya pori tupu. Kufika kule jamaa aliyepewa deal ya kuleta bed akageuza maelezo baada ya kuleta cheupe akaleta cheusi.

Diamond akagoma kushoot alafu zilitumika gharama nyiingi sana kuandaa production kwaajili ya hiyo scene so isiposhutiwa muda huo ile gharama yote inakuwa hasara na mbaya zaidi juwa lilikuwa linazama hata wangesema waende town wakachange ingekuwa nje ya muda na kesho yake ilikuwa tunarudi Dar kumalizia shots za video ya kama utanipenda.

So ilikuwa no way out Diamond lazima ashoot basi wakaanza kumjaza pale washoot hivo hivo tu ‘ Diamond aligoma mpaka mwisho alisema huwa siamini Plan B hata kidogo so i can’t broo. Na wote tukamuona miyeyusho but baada ya video kutoka nimeona faida ya ubishi wake siku ile.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents