Rapper wa Tamaduni Muzik, Azma Mponda na member wa kundi la Chamber Squad, Dark Master wameachia wimbo wa pamoja uitwao We Never Give Up uliotayarishwa na producer wa Mwanza, Mally.
“Tumefanya wimbo mpya mimi na Darkmaster Mwanachemba. Tumefanya pia video yake. Ni maalum kwa wana harakati wote. Miaka 3 nyuma mimi na Kita TheProducer tuliplan kufanya kazi na CHEMBA SQUARD(NGWEA & NOORAH) sisi tukiwa tunaunda UMABE but hatukufanikisha ila wote tulitamani iwe hivyo baada ya mazungumzo, but leo nimefurahi tumefanya kitu na Dark,” amesema Azma kwenye maelezo yake.
“Rest peace COWBOY duniani harakati zinaendelea kama kawa na leo mimi na mwana tumewakilisha CHEMBA SQUARD & UMABE TUMESIMAMA. Sikupanga kuachia wimbo huu mpya kwa sasa but imenibidi niuachie tuu,kwa ajili ya kumuenzi Ngwea na wana wengine waliotangulia.”
Usikilize hapa.