Uncategorized

Tetesi za soka barani Ulaya Jumanne hii Cahill, Chilwell, Mane, Mata, , Fer, Soler

Arsenal wanataka kumsajili beki mkongwe wa Chelsea na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya England Gary Cahill, 33, ili kukabiliana na changamoto ya majeruhi inayoikabili safu yake ya ulinzi.(Mirror)

Gary Cahill

Manchester City wanampango wa kumsajili beki wa Leicester raia wa Uingereza Ben Chilwell, 22, mwishoni mwa msimu. (ESPN)

Tottenham wanapanga kumsajili kiungo raia wa Uhispania anayecheza klabu ya Valencia Carlos Soler, 22, mwishoni mwa msimu. (ESPN)

Sadio Mane

Burnley wanapiga hesabu ya kuwanunua streka Che Adams, 22, kutoka Birmingham na streka wa Tottenham Vincent Janssen, 24. (Mail)

Mchezaji nyota wa Liverpool na timu ya taifa ya Senegal Sadio Mane, 26, amesema kwa sasa Liverpool ndiyo kipaumbele chake, akionekana kupuuzia taarifa kuwa anataka kujiunga na Real Madrid. (World Soccer)

Klabu inayochecha Ligi ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1 Lille wamo mazungumzoni na klabu ya Swansea kumsajili nahodha wao raia wa Uholanzi to sign their Leroy Fer, 29. (Sky Sport)

Juan Mata

Fer pia anawindwa na miamba ya Uturuki klabu ya Fenerbahce. (Mail)

Manchester United wamempatia kiungo raia wa Uhispania Juan Mata, 30, mkataba wa miezi 12 ili kumzuia kuondoka kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu. (Mirror)

Wolves wapo tayari kulipa pauni milioni 18 – ambayo ndiyo rekodi kubwa ya usajili – kumnunua beki raia wa Uhispania Jonny Castro Otto, 24, ambaye kwa sasa anakipiga klabuni hapo kwa mkopo akitokea Atletico Madrid. (Express & Star)

West Ham wamo kwenye mazungumzo na Celta Vigo ili kunua wachezaji wawili; streka wa Uruguay Maxi Gomez, 22, na kiungo wa Slovakia Stanislav Lobotka, 24. (Teamtalk)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents