Habari

Ujerumani yatoa tahadhari ya kimbunga Sabine

Kimbuka cha msimu wa baridi, ambacho kimepewa jina la Sabine nchini Ujerumani, na ambacho awali kilitabiriwa kuvikumba Visiwa vya Uingereza kwa sasa kinatarajiwa kuelekea Kaskazini mwa Ulaya.

The storm flooded streets and squares in the old town near the harbor of Wismar in northern Germany.

Mamlaka imeonya kwamba upepo mkali ambao utatokea Bahari ya Atlantik, utasababisha kimbunga kitakachovuma kwa nguvu ya kilometa 120 kwa saa, mvua kali na mvua zenye ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo ya bara Ulaya.

Kwa mujibu wa chombo cha habari cha DW, Idara ya hali ya hewa ya Ujerumani DWD imesema kimbunga Sabine kinatarajiwa kupiga Kaskazini/Magharibi mwa Ujerumani nyakati za asubuhi ya leo, na kisha kuelekea Kusini mwa Ujerumani na hasa katika jimbo la Bavaria.

Shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa limesema abiria wajiandae na matukio ya kusitishwa kwa safari za ndege.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents