Michezo
Wachezaji wanne ambao ni ‘Target’ ya Man United
Miamba ya soka nchini Uingereza Manchester United inamuwinda kwa udi na uvumba winga wa Borrusia Dortmund, Jadon Sancho, 21 kwenye dirisha la usajili.
Hata hivyo mashetani hao wekundu wamekusudia kusaini moja kati ya nyota hawa watatu, Ousmane Dembele kutokea Barcelona, Cristiano Ronaldo wa Juventus na nyota wa Chelsea, Hudson-Odoi.
Dembele kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na Manchester United, ingawaja usajili huo umeonekana kugonga mwamba lakini taarifa zilizopo ni kuwa United hawajakata tamaa.
United pia wamehusishwa na kuhitaji huduma ya Ronaldo, mara kadhaa wameonekana kama wana nia ya kumrudisha Old Trafford nyota huyo baada ya miaka 12 kupita tangu Mreno huyo alipotimkia Real Madrid.
Na wa mwisho ambaye ni tageti ya Mashetani wekundu ni mchezaji wa mabingwa wa Champions League klabu ya Chelsea mchezaji, Hudson-Odoi.