Uncategorized

Wafuasi wa TB Joshua wakusanyika kanisani kwake kuomboleza (+ Video)

Wafuasi wa Mhubiri wa Nigeria Temitope Balogun Joshua, maarufu TB Joshua wamekusanyinka katika makao makuu ya kanisa la Synagogue Church of All Nations [SCOAN] mjini Lagos kuomboleza kifo chake.

Kifo cha TB Joshua kilichotokea Jumapili Alfajiri kumeiibua maswali mengi huku baadhi ya watu wakitaka kujua kilitokana na nini.

Kanisa la SCOAN halikuthibitisha chanzo cha kifo cha ghafla cha mhubiri huyo.

Dis woman outside di church break down begin cry as she hear di news
Image caption: Waumini walikusanyika katika ukumbi wakanisa hilo baada yakupokea taarifa za kifo cha TB Joshua

Waumini na watu wanaoishi karibu na kanisa hilo walikusanyika kumuomboleza.

“Alikuwa mtu wa Mungu. ISijawahi kuona mhubiri mkarimu anayewasaidia watu hata kama sio wafuasi wa kanisa lake,” Saidat ambaye ni muumini wa dini ya Kiislamu aliiambia BBC.

Nkiru, mmoja wa waombolezaji alisema”Nitamkosa sana. Sijui hili kanisa litaendele vipi baada ya kifo chake.”

Di church environment full wit pipo wey dey cry and lament di death of dia Prophet.
Image caption: Kina mama hao wanaonekana wakiwa na majonzi makubwa baada yakupokea taarifa za kifo cha TB Joshua

Mke wake Evelyn Joshua, mmoja wa wahubiri wakuu wa kanisa la SCOANalielezea kugutushwa na kifo cha ‘’ghafla” cha muwe wake.

“Kumpoteza mwenza sio jambo rahisi; iwe ghafla ua la, inavunja moyo.

“Majonzi huharibu ustawi wetu kwa ujumla. Lakini cha msingi ni kumtumainia Mungu.” Mke wa TB Joshua aliongeza kusema.

Prohpet TB Joshua and im wife, Evelyn Joshua
Image caption: Mhubiri TB Joshua na mke wake , Evelyn Joshua

“Ni yeye tu [akiashiria Mungu] anaweza kutufariji wakati huu mgumu,” alisema mke wa mhubiri huyo.

Taarifa iliotolewa na kanisa lake la SCOAN siku ya Jumapili alfajiri ilithibitisha TB Joshua alifariki akiwa na umri wa miaka 57.

Bofya hapa chini kutazama.

https://www.instagram.com/tv/CP0BD8Nhzzt/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents