Watano kuwania tuzo ya mwanasoka bora BBC Afrika 2015
Wacheji watano ambao wanagombea tuzo ya BBC kwa mwanasoka bora wa mwaka 2015 wametangazwa kwenye hafla maalum iliyoandaliwa mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mshindi wa tuzo hiyo mwaka 2014 Yacine Brahimi, yupo kwenye orodha hiyo pamoja na Pierre-Emerick Aubameyang, André Ayew, kutoka Ghana, Sadio Mané na Yaya wote wa Ivory Coast.
Mshindi ataamuliwa na mashabiki wa soka Afrika ambao watapewa fursa kupiga kura hadi tarehe 30, Novemba.
Unaweza kupiga kura mtandaoni kwa kubofya hapa au kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kwa nambari +44 7786 20 20 08:
Ujumbe 1 kwa-Emerick Aubameyang
Ujumbe 2 kwa André Ayew
Ujumbe 3 kwa Yacine Brahimi
Ujumbe 4 kwa Sadio Mané
Ujumbe 5 kwa Yaya Touré
Mshindi atatangazwa ijumaa tarehe 11 mwezi December wakati wa matangazo maalum kwenye BBC World News na BBC World Service, wakati mitandao ya BBC Sport na BBC Africa ikitoa pia matangazo. Kwa sheria na masharti bofya hapa.
Source:BBC