Picha

Watu 40 wapoteza maisha baada ya lori la mafuta kuwaka moto Kenya

Idadi ya watu waliopoteza maisha baada ya lori la mafuta kugonga magari kadhaa kabla ya kuwaka moto kwenye barabara ya Nairobi-Naivasha nchini Kenya, imeongezeka hadi kufika 40.

n6

Watu wawili walionusurika kwenye ajali hiyo wamelazwa kwenye hospitali ya Nairobi, huku mmoja akiwa amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi.

naivashapic

Mashuhuda waliokuwepo kwenye tukio hilo wamesema dereva wa lori alishindwa kumudu gari lake na kugonga gari jingine na kusababisha magari mengi kugongana. Ajali hiyo iliyotokea kwenye barabara iliyo na shughuli nyingi, kilomita 80 kutoka Nairobi, ilisababisha taharuki kubwa.

n1

Miili mingi kwenye ajali hiyo imeungua kiasi cha kushindwa kutambulika.

n3

n2

Chanzo: Daily Nation Kenya

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents