Wizkid ataja sababu zinazomfanya asishobokee tuzo
Ukijaribu kumfatilia Wizkid utagundua kuwa ni msanii mkubwa wa Afrika ambaye amekuwa akitajwa kuwania tuzo mbalimbali, lakini huwa hajishughulishi kabisa kufanya kampeni ya kuhamasisha mashabiki wake kupiga kura kama wafanyavyo wasanii wengine na matokeo yake tuzo nyingi huwa hashindi.
Staa huyo wa Nigeria ambaye anatarajia kuja Tanzania mwisho wa mwezi huu amemjibu shabiki wa Tanzania aliyemuuliza kama ni kweli hajali kuhusu nominations anazopata kwenye tuzo mbalimbali.
Wizkid alijibu kuwa amekuwa na bokkings za show kila weekend toka mwaka huu umeanza hadi sasa, kwa maana nyingine yuko busy na kutengeneza hela, na kuongeza kuwa ana remix kubwa (Ojuelegba) pamoja na mashabiki wa kweli.
@Fresh120Media I've been booked every weekend from January till date. I got the biggest remix out of the continent and the most amazing fans
— Wizkid Ayo Balogun (@wizkidayo) October 13, 2015