Diamond Platnumz

Diamond Platnumz kuperform jukwaa moja na wakali wa Nigeria Davido na Ice Prince nchini Kenya mwezi ujao (July)

Ni ukweli ulio wazi kuwa star wa ‘Kesho’ Diamond Platnumz ‘anaweza’ kuwa msanii wa Tanzania anayefanya show nyingi zaidi kwa sasa na za gharama kubwa, baada ya kuwachanganya mashabiki wa Comoro na crew yake ya Wasafi weekend iliyopita sasa anategemewa kushare jukwaa moja na wakali kutoka Nigeria Davido na Ice Prince jijini Nairobi mwezi July.

diamonzzz

Diamond Platnumz kipenzi cha mabinti ataungana na star wa Nigeria hit maker wa ‘Dami Duro’ Davido, Ice Prince, Victoria Kimani wa Kenya, na wakali wengine katika ‘Boombaataa Festival’.

Mtandao wa Ghafla umethibitisha ushiriki wa Diamond katika show hiyo kubwa ambayo hufanyika mara moja kwa mwaka nchini Kenya, yenye lengo la kuleta burudani ya utofauti kwa wanamuziki wa Afrika, fashion pamoja na utamaduni.

Show hiyo inategemewa kufanyika (July 27) mwaka huu Nairobi, Kenya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents