Furaha ya ushindi yamfanya Ole Gunnar Solskjaer kukata mitaa kupeleka koti lake kwa dobi, ni lile alilolivaa dhidi PSG
Katika hali isiyokuwa ya kaiwadi kwa watu wenye hadhi na umaarufu mkubwa kupeleka wenyewe nguo zao kwa dobi ‘dry cleaners’, hali hiyo imejitokeza kwa kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer akionekana kukata mitaa huku akiwa ameshikilia koti lake alilovaa hapo jana usiku wakiti akiisambaratisha Paris Saint-Germain pasipo watu kuamini.
Akiwa mwenye furaha usoni huku akitembea kwa kujiamini meneja huyo mwenye kibarua cha muda mfupi ndani ya Man United, Solskjaer alionekana kupeleka suti hiyo baada ya kujipatia heshima kubwa kwa kuitoa PSG ugenini kwa jumla ya 3 – 1 na kunufaika kusonga mbele kutokana na mabao ya ugenini ambayo hufanya matokeo ya jumla kuwa 3 – 3.
Mabao ya Man United yakifungwa na Romelu Lukaku akitupia mawili na Marcus Rashford moja.
Mara baada ya matokeo hayo United ilirejea Uingerea majira ya saa 2: 25 asubuhi ya leo huku Solskjaer akiongoza timu nzima pamoja na benchi la ufundi.