Michezo

Kocha wa Pacquiao anahofia Mayweather ataingia mitini May 2 (Picha)

Kocha wa Manny Pacquiao ana wasiwasi kuwa Floyd Mayweather anaweza asitokee kwenye pambano la kesho kutwa jijini Las Vegas.

2825E46C00000578-3061460-image-a-35_1430343008452
Floyd Mayweather na Manny Pacquiao walikutana jana mbele ya waandishi wa habari jijini Las Vegas

Pacquiao na Mayweather wanakutana Jumamosi hii kwenye pambano lenye gharama kubwa katika historia ya ndondi duniani. Freddie Roach, kocha wa Pac alisema: Nina wasiwasi kama (Mayweather) atakuja usiku huo.

2825E7D300000578-3061460-image-a-41_1430343137572
Mshindi wa pambano hilo atakabidhiwa mkanda huu wa thamani kubwa

“Sidhani kama mabondia wote wanahofia, ila sidhani kama alitaka kupigana. Alilazimishwa kupigana pambano ambalo hakulitaka,” aliongeza.

2826364D00000578-3061460-image-a-78_1430357149893

“Sijui tu kwanini Floyd amekuwa mkimya kwenye pambano hili. Maneno yake yana woga!

2825EAC300000578-3061460-image-a-44_1430343469263

Hata hivyo Mayweather hakushangazwa na kauli ya Roach na kudai: Nitakuwepo. Niliongea uchafu siku za nyuma lakini pambano hili linajiuza lenyewe, hivyo sina haja.”

2825E31F00000578-3061460-image-a-34_1430342965811

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents