Uncategorized
Mzee Akilimali afunguka kuelekea mechi ya Yanga dhidi ya Simba ‘Tunakwenda Taifa kuchukua pointi tatu kutoka kwa mtani’ (+audio)
Katibu wa Baraza la Wazee la klabu ya Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali amesema kuwa siku ya Jumamosi wanakwenda kuchukua pointi tatu kwa mtani wao wa jadi Simba SC kwenye wa ligi kuu soka Tanzania Bara aidha liwe jua iwe mvua huku akihofia kufunguka zaidi kwakuwa wapo baadhi ya watu ambao wanabadili maneno yake na kuandika kitu ambacho hakukisema jambo ambalo linamtengenezea sinto fahamu na Wanayanga wenzake