Picha: Mary J Blige atumbuiza Nigeria katika tamasha la ‘Sisters with Soul‘ jana (Sept 27)
Malkia wa ‘Hip hop Soul’ Mary J Blige alikuwa barani Afrika jana kwa kazi moja tu ya kutumbuiza katika tamasha la muziki lililofanyika Nigeria usiku wa jana.
Mary J (42) ambaye aliwasili Nigeria jana (September 27) kwa private jet aliungana na wasanii wengine wa Nigeria na Afrika katika tamasha la ‘Sisters with Soul‘ lililofanyika Lagos.
Mary J akiwasili Lagos, Nigeria
Mary J akitumbuiza katika tamasha hilo
Victoria Kimani wa Kenya pia ni miongoni wa wasanii walioshare jukwaa moja na MJB kutoka Marekani katika tamasha hilo.
Victoria Kimani katika concert ya Sisters with Soul
Mara baada ya tamasha hilo Blige aliiaga Naija na asubuhi ya leo ametweet kuwashukuru mashabiki wake wa nchi hiyo.
GoodMorning Lagos. Thank U so much 4 the warm welcome, love & support. I had great time with U! Sorry I had to leave so quickly. Love. MJB.
— Mary J. Blige (@maryjblige) September 28, 2013
Picha: 36ng.com, Lailasblog