Videos

Picha/Video: Gorilla aliyeuawa baada ya mtoto kuangukia kwenye zoo azua mjadala duniani

Walinzi wa zoo waliompiga risasi na kumuua gorilla Jumamosi baada ya mtoto wa kiume mwenye miaka minne kuteleza na kuangukia kwenye eneo lenye mawe na maporoko ya maji alilokuwa akitunzwa huko Cincinnati, Marekani wamesababisha mjadala na hasira kali duniani kutokana na uamuzi huo.

https://www.youtube.com/watch?v=Py_1aCt2c0s

Mkurugenzi wa Cincinnati Zoo, Thane Maynard amedai kuwa uamuzi waliochukua kumuua mnyama huyo mwenye miaka 17 aitwaye Harambe ulikuwa sahihi ili kumlinda mtoto huyo aliyekuwa hatarini.

Video zinamuonesha Harambe akimvuta mtoto huyo majini. Waangalizi wa zoo hiyo walimpiga kwa gobole na kumuua. Tukio hilo limesababisha hasira mtandaoni kuhusu kuuliwa kwa Harambe na huku wengine wakiwalaumu wazazi wa mtoto huyo.

“That child’s life was in danger. People who question that don’t understand you can’t take a risk with a silverback gorilla — this is a dangerous animal. Looking back, we’d make the same decision. The child is safe,” alisema Maynard.

34BD01DF00000578-3615783-The_zoo_shot_the_beloved_animal_after_he_dragged_the_boy_through-a-3_1464591377084

Familia hiyo ilienda kutembea kwenye zoo hiyo Jumamosi iliyopita na ndipo mtoto wao alipoteleza na kuanguka kwenye eneo alipokuwa mnyama huyo. Mtoto huyo alichukuliwa na kupelekwa kwenye hospitali ya watoto na kuruhusiwa jioni ya siku hiyo.

Familia hiyo ilitoa shukrani kwa waangalizi wa zoo hiyo.

“We are so thankful to the Lord that our child is safe. He is home and doing just fine. We extend our heartfelt thanks for the quick action by the Cincinnati Zoo staff. We know that this was a very difficult decision for them, and that they are grieving the loss of their gorilla. We hope that you will respect our privacy at this time.”

Baadhi ya watu wanadai kuwa wazazi wa mtoto huyo wanapaswa kukamatwa kwa uzembe wao.

34C650F800000578-3616453-image-a-56_1464634975377

Ombi la mtandaoni (petition) lililopewa jina ‘Justice for Harambe’ limepata sahihi zaidi 100,000 ndani ya saa 48. “This beautiful gorilla lost his life because the boy’s parents did not keep a closer watch on the child,” inasema petition hiyo.

34C655C300000578-3616453-image-a-54_1464633222408

Na sasa mtandao wa Daily Mail umebaini wazazi wa mtoto huyo kuwa mama yake Michelle Gregg, 32 na mume wake Deonne Dickerson, 36, mwanaume ambaye inasemekana ana historia ya matukio ya kihalifu.

34C8870D00000578-0-image-a-1_1464652047487
Wazazi wa mtoto huyo

Makosa aliyowahi kutuhumiwa kufanya ni pamoja ujambazi, makosa ya kutumia silaha za moto, biashara ya madawa ya kulevya na mengine.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents