Siasa

Raila Odinga apata mwaliko kutoka kwa Rais wa Marekani Barack Obama kuja Tanzania kukutana naye

Hivi karibuni kulizuka mjadala juu ya ujio wa Rais wa Marekani Barack Obama nchini Tanzania bila kwenda nchi jirani ya Kenya. Taarifa za sasa inaonekana waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga amepata mwaliko rasmi kutoka kwa Obama kuja kufanya naye mkutano Tanzania.

U.S. President Barack Obama and First Lady Michelle Obama With World Leaders at the Metropolitan Museum in New York

Taarifa iliyotolewa na mtandao wa Daily Post wa Kenya inasema Odinga amepata mwaliko huo kutoka kwa Obama alipokuwa anaelekea Afrika Kusini wiki iliyopita katika World class democracy forum ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya Afrika.

Bwana Odinga anatarajiwa kutumia private Jet itakayokodishwa na US State Department kwaajili ya kusafirisha viongozi maarufu akiwemo katibu mkuu wa umoja wa mataifa Kofi Annan kuja Tanzania.

Rais Obama anategemea kuitembelea Tanzania mwezi ujao (July) ikiwa ni moja ya nchi tatu za Afrika ambazo anategemewa kuzitembelea. Nchi nyingine ni South Africa na Senegal.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents