Technology

Simu mpya TECNO SPARK 4 ni moto; Kamera 3 nyuma, GB 32, kioo nchi 6.52 ni balaa (+video)

Dar Es Salaam Tanzania, 1/10/ 2019 hii leo kampuni ya TECNO imewapa tena wateja wake nafasi ya kufurahia ladha mpya ya simu janja na ya kipekee hii ni kutokana na ujio wa simu mpya ya TECNO Spark4 yenye sifa lukuki na kwa bei nafuu.

Akizungumza na vyombo vya habariwakati wa uzinduzi wa TECNO Spark 4 uliyofanyika katika duka jipya la TECNO ‘TECNO Smart Hub Karia Koo Manager wa masoko wa kampuni ya Tecno, Bwana William Motto amesema Teknolojia ya AI iliyopo ndani ya Tecno Spark 4 imebeba uwezo mkubwa wenye kuzipa ‘support kamera tatu za nyuma za Tecno Spark 4 kwa picha nzuri na video zenye ubora.

William Motta amevieleza vyombo vya habari kuwa TECNO Spark 4 imekuja na sifa zifuatazo kasi ya mtandao wa 4G, Kamera tatu za nyuma, G32 zenye memory na Kioo cha Nchi 6.52 super full-view.

Wakati Mkumbo Mvonga kutoka kitengo cha Tigo Device amesema pindi unaponunua simu ya Tecno Spark 4 hapo hapo utazawadiwa ofa ya GB 18 kutoka kwao. Uzinduzi wa simu hii mpya unakwenda sambamba na ofa hiyo.

TECNO Spark 4 inapatikana katika maduka yote ya TECNO na Tigo nchinina hizi ni baadhi ya sifa za Tecno Spark 4. Megapixel 13+2 nyuma, GB 32 + GB2 Ram, 4000bettery, Kioo cha Nchi 6.52 na Warranty ya miezi 13.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents