Solskjaer kukabidhiwa rasmi Manchester wiki hii, rekodi hii bora aliyoweka United yawa sababu
Manchester United ipo mbioni kumpa kandarasi ya moja kwa moja kocha wake Ole Gunnar Solskjaer baada ya kuhudumu nafasi hiyo kama mwalimu wa muda akirithi nafasi ya Jose Mourinho.
Licha ya kukumbana na ugumu kwenye mchezo wa hapo jana usiku, inafahamika kuwa Solskjaer atapata mkataba wa kudumu wiki hii.
Kocha huyo mwenye umri wa mika 46, raia wa Norway mpaka sasa ameweka rekodi bora kabisa ya kushinda jumla ya michezo 14 kati ya 19 aliyosimamia klabu hiyo tangu kuchukua nafasi ya Jose Mourinho mwezi Desemba.
United siku zote imekuwa ikisema kuwa itafanya maamuzi kabla ya kufika mwishoni mwa msimu lakini huwenda akatangazwa mapema mnoo.
Kwa sasa Solskjaer yupo na familia yake nchini Norway akipisha kipindi hiki ambacho wachezaji wakitumikia timu zao za taifa.