Uncategorized

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatatu hii, Mbappe, Marcelo, Henry, Giroud

Kiwango cha mshahara anachokitaka kiungo wa Manchester United Paul Pogba, 26, kinaweza kikawa kikwazo kwa Real Madrid kumsajili nyota huyo raia wa Ufaransa. (AS)

Image result for pogba

Chelsea wannapiga hesabu za kumnyakua kiungo wa Brazil na klabu ya Barcelona Philippe Coutinho, 26, kama mbadala wa mshambuliaji wao raia wa Ubelgiji Eden Hazard, 28, ambaye mwisho wa msimu anatarajiwa kuhamia Real Madrid.(Calciomercato)

Klabu ya Manchester United ipo tayari kumpandisha Mike Phelan mpaka kuwa mkurugenzi wa ufundi, na nafasi yake ya meneja msaidizi kupewa kiongo wa zamani wa klabu hiyo Michael Carrick. (Mail)

Mchezaji nyota wa zamani wa Arsenal ambaye pia alitimuliwa kwenye kazi ya ukufunzi na klabu ya Monaco, Thierry Henry, 41, yumo kwenye mazungumzo na klabu ya New York Red Bulls ya ligi ya soka Marekani ili kujiunga nao kama mkufunzi. (Sky Sports)

Mshambuliaji nyota wa Ufaransa na klabu ya PSG Kylian Mbappe, 20, amekanusha uvumi ulioenea kuwa ana mpago wa kuhamia Real Madrid. Mbappe ametoa kauli hiyo baada ya kuifunga goli tatu timu yake ya zamani Monaco. (Goal.com)

Beki raia wa Brazil Marcelo, amesisitiza kuwa hana mpango wa kuihama klabu yake ya Real Madrid mwishoni mwa msimu – licha ya uvumi kuenea kuwa mchezaji huyo alikuwa akitammani kuungana tena na Cristiano Ronaldo, katika klabu ya Juventus. (Bein Sports, via Mirror)

Marcelo
Image captionMarcelo (kulia) ameamua kuuzima uvumi kuwa anajipanga kuhamia Juventus mwishon mwa msimu.

Kocha wa muda mrefu wa wachezaji chipukizi wa Aston Villa Sean Kimberley ameikacha klabu hiyo. (Birmingham Mail)

Bosi wa Newcastle Rafa Benitez amedai kuwa mfumo wa mishahara wa klabu hiyo unaifanya timu isiwe na matokeo mazuri kwenye Ligi ya Premia. (Newcastle Chronicle)

Rafa Benitez
Image captionRafa Benitez amekuwa akihusishwa na mipango ya kuihama Newcastle

Mshambuliaji wa Newcastle raia wa Uhispania Ayoze Perez, 25, ameashiria kuwa anataka kuihama klabu hiyo mwushoni mwa msimu. (Mirror)

Rais wa klabu ya Nice ya Ufaransa Gauthier Ganaye amesema klabu yake huenda ikamsajili mshambuliaji wa Chelsea Olivier Giroud, 32. (Goal.com

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents