Bongo5 Exclusives

Uchaguzi wa Papa: Bado ngoma nzito, moshi mweusi watoka tena siku ya 2

Makardinali wa kanisa katoliki dunia wameshindwa kumchagua Papa mpya katika siku ya kwanza na ya pili ya mkutano wao mjini Vatican.

papal-conclave

Makardinali hao wanakutana kwa siku ya pili leo kumchagua mrithi wa Papa Benedict, aliyejiuzulu mwezi uliopita.
Kura zingine zitapigwa baadaye mchana. Moshi mweusi ulionekana ukitoka kwenye paa la kanisa Sistine kuonesha kuwa kura hazijatosha kumpata Papa mpya na wa 266.

smoke

Ukitoka moshi mweupe ni ishara kuwa Papa mpya amepatikana.

Baadhi ya wananchi kutoka mataifa mbalimbali duniani wakifualitia kwa ukaribu mkutano huo wa Vatican
Baadhi ya wananchi kutoka mataifa mbalimbali duniani wakifualitia kwa ukaribu mkutano huo wa Vatican

Makardanali hao 115 watapiga kura mara nne kila siku hadi theluthi mbili yao wampigie kura mmoja. Miongoni mwa makardiinali wanaotajwa kuwa na uwezekano wa kushika wadhifa huo ni pamoja na Angelo Scola wa Italia, Odilo Scherer wa Brazil na Marc Ouellet wa Canada.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents