Unai Emery aomba radhi kwa shabiki aliyempiga na chupa ya maji
Kocha wa Arsenal, Unai Emery amewaomba radhi mashabiki wa klabu ya Brighton baada yakumpiga na chupa mmoja kati ya mashabiki wa timu hiyo kwenye mchezo uliyomalizika kwa sare ya bao 1- 1.
Muhispania huyo aliipiga teke chupa ya maji na kumrukia mmoja wa mashabiki waliyokuwa uwanjani hapo na kuomba radhi muda huo huo kwa kitendo hicho.
Kwenye tukio hilo, Emery alionekana kwenda upande wa mashabiki na kumuomba radhi yule aliyoguswa na chupa hiyo.
Baada ya mchezo kocha huyo alielezea kile kilichotokea ‘’Niliwaambia samahani, kwasababu nilipiga teke chupa iliyompata shabiki mmoja baada ya kuvunjika moyo kwa matokeo yalivyokuwa yanaonekana dakika za mwisho,’’ amesema Emery.
Unai Emery ameongeza ‘’Haikuwa nzito, lakini ilimgusa mmoja kati ya mashabiki na niliwaomba radhi.’’
Mesut Ozil aliingia kwenye kipindi cha pili lakini ameshindwa kuisaidia Arsenal kupata matokeo.