Uncategorized

Ushindi mbele ya Bayern Munich wampa kiburi Jurgen Klopp, akunwa na bao la Mane ‘Bao la kwanza nitalitazama zaidi ya mara 1,000’

Mara baada ya kupata ushindi wa mabao 3 – 1 mbele ya wenyeji Bayern Munich meneja wa klabu ya Liverpool, Jurgen Klopp amekisifia kikosi chake kwa kazi kubwa waliyofanya hadi kutinga hatua hiyo ya robo fainali ya Champions League huku akiamini kuwa ulikuwa usiku uliyobora kwa upande wake na wapo tayari kwa anayekuja mbeleyao.

Mabao mawili yaliyofungwa na Sadio Mane na moja likifungwa na Virgil van Dijk yalitosha kuihakikishia Liverpool nafasi ya kutinga hatua hiyo ya robo fainali na kujumuika na klabu nyingine za Uingereza ambazo ni Spurs, Man United pamoja na Man City huku kutinga kwa timu zote hizi nne za taifa hilo kunaifanya kuwa ni kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2008/9.

Klopp also praised defender Virgil van Dijk after his headed goal during Wednesday's game

‘Kwenye mechi kama hii, huwezi kupumzika, hakika tulistahili ushindi. Ni vigumu kucheza ugenini dhidi ya Bayern Munich kwakuwa ni timu kubwa lakini najivunia mno kwa kile kilichofanywa na vijana wangu,” amesema Klopp.

”Jordan Henderson amejitonesha jeraha lake lakini natumaini hatokuwa sana, bao la kwanza nitatamani kuliangalia zaidi ya mara 1,000. Sehemu ya ulinzi ilikuwa ikovizuri na hatukujilinda kama vile tunavyofanya siku zote kwenye michezo yetu ya ugenini, Virgil van Dijk ametupatia muunganiko mzuri hasa kwenye mipira iliyokufa na nihatari.”

Klopp revealed that Jordan Henderson had twisted his ankle when he was forced off

”Nilijua tungepata nafasi lakini sikuwa na uhakika kama ingetokea, lakini vijana wangu wameitengeneza na ilikuwa kitu kizuri kwetu.”

”Sikutaka kuishushia kichapo Bayern, lakini nilihitaji ushindi kwa Liverpool. Ninahakika nitakuwa na mashabiki wengi wenyefuraha kutoka Dortmund na kama nitaweza kuwasaidia basi itakuwa bora pia.

Klopp amekuwa na kikosi bora kabisa katika ulimwengu wa soka ikiwa ni pamoja na aina ya uchezaji wao kuwa mzuri na kuifanya Liverpool kupiga hatua kubwa kwenye maendeleo ya soka la ushindani tangu alivyokabidhia timu hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents