Video: Makundi yanajenga umoja – SSK
Kundi jipya la muziki wa Hip Hop Bongo, ‘Sisi Sio Kundi (SSK)’ wamebainisha uwepo wa makundi katika muziki kuna jenga umoja na ushirikiano.
Member wa kundi hilo P the MC ameimbia Bongo5.com kutoka na yeye kujua hilo amejikuta katika historia ya kufanya kazi na watu (makundi) ili aweze kupata hamasa ya kufanya kazi kubwa zaidi.
“Unajua mnapokuwa mtu zaidi ya mmoja mnafanya kazi mnashare mawazo, ina maana kuna vitu Wakazi anaweza kuwa anafahamu lakini kama tusingekuwa pamoja nisingeweza kuvipata lakini nimeweza kuvijua,” amesema P the MC.
Katika hatua nyingine wamebainisha kuwa albamu yao ipo tayari na pindi itapokua tayari itapatikana katika mfumo wa hard Copy na soft copy, na imeshirikisha wasanii wakubwa ambao kwa sasa ni mapema kuwataja. Itazame interview nzima hapa chini.
By Peter Akaro