Burudani

Uzinduzi wa Wonder Woman wakwama

Kufuatia tukio la kigaidi liliotokea nchini Uingereza katika mji wa Manchester kwenye ukumbi wa Mancherster Arena na kusababisha vifo vya watu wapatao 22 na 59 kuwa majeruhi, waandaji wa filamu ya Wonder Woman wamesitisha uzinduzi wa filamu hiyo.

Filamu hio ambayo ilitarajiwa kuoneshwa Mei 31 kwa mujibu wa Director Patty Jenkins, imesogezwa muda hadi Juni 1 mwaka huu.

Juni 2 filamu hiyo itazinduriwa rasmi nchini Marekani licha ya kuwa Alhamisi hii itatazamwa katiaka jiji la Los Angeles.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza, waandaaji wa filamu hiyo, Warner Bros wamesema kuwa wamekatisha uzinduzi huo kutokana na tukio la kigaidi liliotokea siku ya Jumatatu katika tamasha la Dangerous Woman la msanii Ariana Grande kwenye ukumbi wa Manchester Arena.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents