Habari
Mama Janeth Magufuli atoa msaada wa chakula kwa wafungwa (+video)
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Janeth Magufuli ametoa msaada wa chakula kwa wafungwa wa gerezani la Ukonga huku akiwataka Watanzania kuachana na dhana potofu kwamba wafugwa waliopo gerezani ni wahalifu.
Mama Janeth amekabidhi mchele Tani 4.8, Unga wa mahindi Tani 4.8, sukari Tani 2.8 pamoja na tende.
Pamoja na kutoa msaada huo, Mama Janeth amewatakiwa Waislam wote nchini mfungo mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na kuwataka katika kipindi hiki cha mfungo wasisahau kuliombea Taifa amani.