Michezo
Messi arejea Barcelona na gundu, wapigwa nyumbani ‘Camp Nou’ kipigo cha rekodi na vibonde wa La Liga
Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi amerejea kwenye kikosi hicho kwa mara ya kwanza tangu avunjike kiwiko kwa klabu yake kupigwa goli 4-3 kwenye uwanja wao wa Nou Camp dhidi ya Real Betis.
Magoli ya Barcelona yamefungwa na Lionel Messi x2 na Arturo Vidal huku Ivan Rakitic akipigwa umeme kwenye mchezo huo.
Kwa matokeo hayo, Barcelona wanaendelea kuongoza ligi kwa alama 24 tofauti ya alama 1 dhidi ya Atletico Madrid wenye pointi 23.
Huu unakuwa mchezo wa kwanza kwa Barcelona kupigwa nyumbani tangu walipofungwa na Alavés mwaka 2016 kwenye mchezo wa ligi.