Habari
Idris Elba arekodi album kumuenzi Mandela
Muigizaji wa Uingereza, Idris Elba amerekodi album maalum ya kumuenzi Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Muigizaji huyo mwenye miaka 41 ameigiza kama Mandela kwenye filamu ya Mandela: Long Walk To Freedom.
“Album itaitwa ‘Mi Mandela’. Nilienda tena Afrika Kusini na nimefanya kazi na wanamuziki wakubwa. Najivunia sana kuwa na album hiyo. Ntasubiri mpaka filamu iishe utamu ili isiathirike lakini nitaitoa mwakani. Kimsingi, ni barua ya upendo kwa Mandela kuhusu mimi kumuigiza,”Elba.