Burudani
Aunty Ezekiel adai hajutii kuwa na Mose Iyobo
Muigizaji wa filamu, Aunty Ezekiel amesema anajisikia fahari kuwa mpenzi na mzazi mwenzake na Mose Iyobo na kwamba hajutii kuwa naye.
Aunty ambaye alipanda kwenye jukwaa katika show ya Diamond na Wizkid weekend iliyopita na kumtunza Moses ambaye ni dancer wa hitmaker huyo, ameiambia Bongo5 kuwa anampenda mpenzi wake ndio maana anamsupport katika kila anachokifanya.
“Yaani kwa kifupi najikuta sijutii kumpenda na hata ninachokifanya kwake,” amesema. “Nimeamua kumpenda na kazi anayofanya ni kama kazi za watu wengine, ni kama watu wa ofisini. I am happy kuwa na kazi yake na ninapenda kuwa naye pamoja muda wote. Pia namsupport kwenye shughuli zake, yule ni wangu,” amesisitiza Aunty.