Michezo
Azam FC wametupwa nje kuendelea na michuano ya CAF
Klabu ya Azam FC ambao walikuwa ni wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika wametupwa nje ya michuano ya hiyo baada ya kufungwa kwa magoli 3-0 na Esperance ya Tunisia kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa Tunis, Tunisia.
Azam hadi kipindi cha kwanza kinamalizika timu zote walikuwa hawaja fungana kipindi chapili dakika ya 49 Esperance walipata bao la kuongoza lililopachikwa kambani na Saad Bguir kisha Jouini akaiandika bao la pili na Ben Yousef akaihakikishia timu yake kusonga mbele baada ya kufunga bao la ushindi dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika.