Burudani
Babuu wa Kitaa apata mtoto
Msanii wa Bongo Flava na mtangazaji wa Clouds Media, Babuu wa Kitaa amejaliwa kupata mtoto.
kupitia mtandao wa Instagram rapper huyo ameandika “Welcome to the world Sister duu wangu.#NAHLA”. Baada ya muda mfupi mdogo wake ambaye pia msanii, Country Boy alimpa pongezi Babuu kwa hatua hiyo.
“Hongera BROTHER @babuuwakitaa KARIBU KATIKA DUNIA YA VIUMBE MBALI MBALI #NAHLA” aliandika.
Mwishoni mwa July mwaka huu Babuu wa Kitaa alifunga ndoa shughuli iliyohudhuriwa na watu wake wa karibu wakiwemo watangazaji wenzake na wasanii.