Habari
Barabara za Dar kuanza kujengwa – RC Chalamila
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema ni kweli barabara nyingi zimeharibika Dar es salaam lakini amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na usikivu wakati huu wa mvua nyingi na kwamba mvua zikipungua ujenzi wa barabara hizo utaanza. “Tunajipanga ili tuweze kuingiza magreda hivi karibuni mara baada ya mvua hizi kupungua lakini jambo zuri muda sio mrefu barabara zifuatazo zitatangazwa ili ziweze kupata Wajenzi, Jimbo la Ilala peke yake barabara zipatazo KM 20.9 zitaanza kujenga” “Kariakoo itakua KM 7.8 , Upanga KM 4.6, Ila KM 8.5, Ukonga barabara kubwa ya Banana, Kivule, Kitunda, Msongola itajengwa kwa kiwango cha Lami kwa KM 12.97”
CC: Millard Ayo
Imeandikwa na Mbanga B.