Rais wa Marekani Joe Biden amesema jana Jumapili kwamba, watu wanapaswa kuwa waangalifu dhidi ya ugonjwa wa homa ya nyani ambao unaweza kuwa na athari kubwa ikiwa utaeenea zaidi.
Visa kadhaa vimegunduliwa Marekani na Ulaya mapema mwezi huu na kuzusha wasiwasi.
Watu wengi hupona katika wiki kadhaa baada ya kuambukizwa homa ya nyani. Shirika la Afya duniani limesema kufikia jana Jumamosi kulikuwa na visa 92 vilivyothibitishwa vya ugonjwa huo katika nchi ambazo si kawaida kukutana na ugonjwa huo.