Habari
Bosi wa zamani wa NIDA na wenzake wafutiwa mashtaka
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Ernest Maimu na wenzake wote wamefutiwa mashtaka yao yote baada ya DPP kukosa nia ya kuendelea na kesi yao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Oktoba mwaka jana, Maimu alifutiwa kesi moja ya Utakatishaji Fedha na kusalia na Mashtaka ya Uhujumu Uchumi, kuisababishia Serikali hasara na Matumizi mabaya ya Madaraka