Bongo5 Exclusives
Breaking: Dar Express, Arusha – Dar lateketea kwa moto
Habari zilizotufikia muda mfupi uliopita zinadai kuwa basi la Dar Express lililokuwa linatokea Arusha kuja Dar es Salaam limeteketea lote kwa moto katika eneo la Segera, Tanga.
Inadaiwa kuwa abiria wote wamenusurika lakini mizigo yote imeteketea kwa moto.
“Breaking News!!! Happening n Segera nw, Duh! Wale wa Rombo,mwika, marangu na kilimanjaro kwa ujumla nafikiri hili ni pigo kwetu… Mungu awe ameepusha vifo tu,” ameandika mtu mmoja kupitia Facebook.