Habari
Bunge lampitisha Kassim Majaliwa kwa kura zote kuwa Waziri Mkuu
Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa amethibitishwa na Bunge kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania baada ya kupata kura 350 kati ya kura 350 zilizopigwa sawa na asilimia 100. Majaliwa anashika wadhifa huo kwa kipindi cha pili (2020-2025).