Chelsea yavuliwa ubingwa wa Capital One na Stoke City
Matokeo mabaya yanaendelea kumuandama kocha Jose Mourinho msimu huu baada ya vijana wake wa Chelsea kuvuliwa ubingwa wa kombe la Capital One na Stoke City kupitia mikwaju ya penati kwenye mechi iliyochezwa Jumanne hii.
Stoke City walipata goli lao la kwanza kupitia mchezaji wao Jonathan Walters dakika chache baada kipindi cha pili. Lakini Loic Remy aliyeingia kuchukua nafasi ya Diego Costa aliyetoka baada ya kuumia, aliisawazishia goli Chelsea katika dakika ya 90.
Stoke wamesonga mbele kwenye raundi ya tano ya michuano hiyo kwa ushindi wa penati 5-4 kufuatia sare ya kufungana goli 1-1.
Winga wa kimataifa wa Ubelgiji Eden Hazard alikosa penati iliyoifanya Chelsea kutupwa nje ya mashindano hayo.
Kuvuliwa huko kwa ubingwa kwa Chelsea ni habari mbaya kwa kocha Jose Mourinho ambaye hana kwa sasa. Sasa anasubiri hatima yake dhidi ya Liverpool Jumamosi ijayo kuona kama ataendelea kuwa meneja wa Chelsea.