Michezo

David Moyes afungiwa mechi moja na FA

Kocha wa Sunderland David Moyes amepigwa marufuku mechi moja na chama cha soka cha England kwa kutumia lugha ya matusi dhidi ya mwamuzi wa mechi amepigwa na faini ya £8,000.

39d7652100000578-3897342-image-a-53_1478089106440

Kisa hicho kilitokea baada ya refa kunyima Sunderland mkwaju wa penalti dakika ya 90 mechi ya Jumatano wiki iliyopita ambapo klabu hiyo ilifungwa 1-0 na Southamptn Kombe la FA.

Baada ya mechi hiyo, Moyes alisema: “Tatizo lilitokea aliponiandama hadi pahala nilipokuwa nimesimama. Nilitumia lugha ya matusi na sikufaa kufanya hivyo.”

Moyes tokea ameteuliwa kuwa meneja wa Sunderland Julai na ameshinda alama mbili pekee kutoka katika mechi 10 za ligi.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents