Michezo
Declan Rice – Tutafanya Maajabu
Kiungo Mkabaji wa Arsenal, Declan Rice baada ya kikosi chao kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Aston Villa ameeleza kuwa bado wananafasi ya kupambana kujiweka katika nafasi ya kutwaa ubingwa wa EPL huku akisisitiza kuwa wako tayari kufanya lolote linalowezekana kufanyika. “Bado haijaisha, tuko katika nafasi ambayo siyo ya kuaminika, bado tuko tayari, bado tunazingatia kikamilifu kile tunachotaka kufanya na kile tunachoweza kufanya. “Kutakuwa na misukosuko mingi zaidi katika ligi kuu lolote linaweza kutokea,” Rice.
Imeandikwa na Mbanga B.