Diamond Platnumz
Diamond na Ommy Dimpoz kesho kuchuana na Sauti Sol, Bebe Cool kwenye #HiPipoMusicAwards za Uganda
Tuzo za muziki za nchini Uganda, HiPipo Music Awards zitafanyika Jumamosi hii jijini Kampala, Uganda.
Katika tuzo hizo, Diamond Platnumz na Ommy Dimpoz wanawania kipengele cha wimbo bora wa Afrika Mashariki.
Wawili hao wanachuana na nguli wengine wa muziki kutoka Kenya, Uganda na Rwanda.
Hizi ndio nyimbo zinazowania kipengele cha wimbo bora wa Afrika Mashariki:
• Tayali – Urban Boys Ft Iyanya
• Sitya Loss – Eddy Kenzo
• Ndagushima – Ommy Dimpoz
• Number One – Diamond Platnumz
• Nishike (Touch Me) – Sauti Sol
• Love You Everyday – Bebe Cool
• Kioo – Jaguar
• Baramushaka – Knowless