Michezo
Dube aifuta Azam FC
MAMBO yanazidi kupamba moto kwenye sakata la mshambuliaji, Prince Dube ambaye ameamua kufuta utambulisho wa timu ya Azam FC kwenye akaunti yake ya mitandao ya kijamii ‘Instagram’. . Dube ambaye anahusishwa kujiunga na Yanga, mbali na kuondoa utambulisho huo amefuta picha zote zenye jezi za timu hiyo na kuacha zile za maisha ya kawaida, sambamba na za timu alizopita miaka ya nyuma.