Michezo

Everton kutua Bongo Julai, Je ni Simba au Yanga kucheza nao?

Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter wa klabu ya soka ya Everton, umethibitisha kuwa klabu hiyo kuwasili nchini mwezi Julai na itakuwa ni timu ya kwanza inayoshiriki Ligi kuu nchini Uingereza kucheza na timu za Afrika mashariki.

Ujio wa Everton ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi, Vilabu vinavyo tarajiwa kunufaika na ujio huo ni vile ambavyo vipo chini ya udhamini wa kampuni ya Michezo ya kubashiri ya SportPesa. Kwa hapa nchini mpaka sasa kampuni hii imeingia mkataba na klabu tatu ambazo ni Simba SC, Yanga SC pamoja na Singida United .

 

Kwa mujibu wa Kampuni ya SportPesa, wameandaa ligi ijulikanayo kama SportPesa  Super Cup , inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi tarehe 5  / 6 / 2017, kwa kushirikisha jumla ya timu 8  kutoka mataifa mawili, Tanzania na Kenya, na mshindi wa mashindano hayo atacheza na timu inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza.

Mshindi wa michuano hiyo mikubwa atapata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu thelathini (USD 30,0000) na mshindi wa pili wa michuano hiyo anatarajia kupata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu kumi (USD 10,000).

Kutokana na kuthibitisha kwa klabu ya Everton bilashaka mshindi wa mashindano hayo atacheza na klabu hiyo kongwe iliyoanzishwa  mwaka 1978.

 BY HAMZA FUMO

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents