Burudani
Filamu ya Will Smith ‘Suicide Squad’ yavunja rekodi ya box office kwa kuingiza $250m
Filamu mpya, Suicide Squad imevunja rekodi kwa kuingiza dola milioni 135.1 kwenye majumba ya sinema Marekani katika wiki yake ya kwanza na dola milioni 250 ukiunganisha na mauzo ya dunia nzima, kwa mujibu wa BoxOffice Pro.
Kabla ya Suicide Squad, Guardians of the Galaxy ya mwaka 2014, ndiyo ilikuwa inashikilia nafasi hiyo kwa kuingiza dola milioni 93 katika wiki yake ya kwanza.
Filamu hiyo ina mastaa kibao wakiwemo Will Smith, Jared Leto na Margot Robbie.