Michezo
Gary Neville Kustaafu
Beki mkongwe wa klabu ya Manchester United Gary Neville anajiandaa kufuata nyao za kipa wa klabu hiyo Edwin Van Der Sar,ambaye atastaafu mwisho wa msimu huu.
Neville(35) hakupata bahati ya kupewa mkataba mwingine baada ya kusumbuliwa na majeruhi na hivyo kumfanya acheze mechi tatu tu katika kikosi hicho cha kwanza.
Wakati nyota mwingine waliokuwa wanakipiga Manchester United,Ryan Giggs amefikisha umri wa miaka 37 wiki iliyopita, huku Paul Scholes akifurahia mchezo huo wa soka nchini India.